KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Monday, April 2, 2012

MTOTO WA MCHUNGAJI MHE.JOSHUA NASSARI HATIMAE NDOTO YAKE YAKUINGIA MJENGONI DODOMA YATIMIA.

Siku Za Nyuma niliwahi ona Maono kuwa nimekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, na ndoto hii imekuwa ikinisumbua mno, nilipokuwa nashiriki nilijua nitashinda na hata mwaka 2010 nilijua nitashinda lakini CCM walichakachua matokeo, ninajua Haki ya Mtu huwa haipotei ila inacheleweshwa, kwa sasa Namshukuru Mungu Kwa Ushindi huu, leo ndoto yangu imetimia". Maneno hayo yamesemwa na Mbunge Mchaguliwa katika Jimbo la Arumeru Mashariki Mh.Joshua Nassari
Mh.Joshua Nassari Mbuge wa Arumeru Mashariki.


Akitangaza matokeo hayo ya uchaguzi msimamizi wa uchaguzi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru, Gracias Kagenzi, alisema kuwa Mgombea Ubunge wa Joshua Nassari CHADEMA amepata jumla ya kura 32,972, na huku mpinzani wake mkubwa, Sioi Sumari wa Chama cha Mapinduzi (CCM) akipata jumla ya kura 26,757.
Mpinzani wake alikuwa akichuana nae Bwana Siosi Sumari wa Chama cha Mapinduzi.
Kwamatokeo hayo yanafanya idadi ya Kura zilizompa ushindi Nassari wa Chadema kuwa kura 6,215 dhidi ya Sioi Sumari CCM.
Aidha Kagenzi ametangaza matokeo ya wagombea wengine ambao walishiriki uchaguzi huo kupitia vyama vyao vya Siasa nchini ambapo AFP wamepata kura– 139, DP -77, NRA – 35, SAU – 22, UPDB – 18 na TLP – 18.

Blog hii inampongeza Mh. Joshua Nassari kwa ushindi Mkubwa.

ULIMI MZURI
Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo (Mithali 15:4).
Mithali 4:20-22 inatuonyesha umuhimu wa kulipa Neno la Mungu umakini mkubwa katika maisha yetu; inasema: “Mwanangu, sikiliza maneno yangu…Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote.” “Safi,” kama ilivyotumika katika mstari wetu wa ufunguzi imetafsiriwa kutoka katika neno la Kiebrania “marpe,” ambalo maana yake ni uponyaji. Ni neno hilo hilo lenye tafsiri ya “afya” katika Mithali 4:22. Kwa hiyo, ulimi safi au “ulimi ulio “marpe” ni ulimi uponyao; ulimi unenao afya, uponyaji na uzima!

Sasa, ulimi unaweza kuwa wa uponyaji au wenye dawa pale unapokuwa umejazwa na Neno la Mungu!

Kumbuka, tumesoma katika Mithali 4:22 kwamba Neno ni afya (dawa) katika nyama au mwili wa mwanadamu. Hivyo ulimi unenao Neno la Mungu; ulimi mzuri; hunena afya, rutuba, ustawi na uzima katika mwili. Vile vile utagundua kwamba andiko hilo hilo linasema “…ukorofi wa ulimi huvunja moyo.” Ukorofi maana yake ni uharibifu au udanganyifu; ina maanisha kutokuwa na msimamo na kuchanganya maneno. Huitwa “kupingana” katika ulimi, na husababisha uharibifu au kidonda katika roho.

Wengi bila kujua huchubua au huumiza roho zao kwa kuongea vibaya pale maneno yao yanapokuwa hayaendani na jinsi Injili isemavyo. Roho ya mtu inapokuwa imechubuliwa sana kupitia maungamo mabaya, muda mfupi tu ujao, utajidhihirisha katika mwili. Michubuko au magonjwa mengi yanayopitia katika miili yao yalianzia katika roho zao.

Hii ndiyo maana kama mtoto wa Mungu, unatakiwa kupalilia ulimi ulio mzuri; jifunze kunena Neno la Mungu kwa ujasiri. Moja ya huduma ya Roho Mtakatifu katika maisha yako ni kutakasa maneno yako ili uweze kuwa na “marpe” au ulimi mzuri; ulimi ulio wa uponyaji! Ruhusu huduma hii ijidhihirishe moja kwa moja katika maisha yako; nena Neno la Mungu, na litumie Neno ili kuamua afya yako, mstakabali, mafanikio na ulinzi.

Ukiri

Maisha yangu ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, na ninatembea katika haki, ushindi, mafanikio, afya, ustawi na ukuu. Neno la Mungu limezaa afya ndani yangu; mimi ni ushuhuda wa neema na utukufu wa Mungu kutokana na adhari ya Neno katika maisha yangu. Haleluya!

somo zaidi:Mithali 18:21; Yakobo 3:2

KUJISOMEA MAANDIKO KILA SIKU

Mpango wa kusoma Biblia kwa mwaka 1 : Yoshua 10-12;Luka Mtakatifu 9:1-17

Mpango wa kusoma Biblia kwa miaka 2 : Warumi 2:16-29; Zaburi 65-67

–Christ Embassy International

AThe VOICE warekodi Live DvD Album



Usiku wa jana  kuanzia saa tatu usiku katika ukumbi wa Jumba la Makumbusho unaotazamana na chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es salaam. Kundi maarufu la muziki wa injili liimbalo kwa mtindo wa Akapela lijulikanalo kama THE VOICE, lilikuwa likirekodi LIVE DVD Album. Kwa yeyote Yule aliyefika ukumbini hapo atakubaliana na Hosanna Inc kuwa vijana hawa wanavipaji vya tofauti katika kumtukuza Mungu.

Kundi hili linaloundwa na vijana watano ambao kati yao wanne wanatoka katika familia moja,lilianza kuimba nyimbo ya kwanza iliyopokelewa kwa shangwe ukumbini hapo iitwayo KWENYE MAVUNO, kisha wakaimba nyimbo yao maarufu NAJIVUNIA YESU WANGU ambayo waliimba kwa lafudhi ya Kimasai.Kabla The Voice hawajapanda jukwaani Mc wa shughuli hiyo Minister Godwin Gondwe, aliwakaribisha wageni wote waalikwa kisha shughuli akaanza.Hii ni moja kati ya Live DvD album ambayo ikitoka hutakiwi kuikosa.

The Voice wakiwasalimia mamia ya watu waliojitokeza 


 ukumbini hapo
 Hii pia ni sehemu ya watu waliojitokeza katika live 


 recording ya vijana hawa wa The Voice

The Voice wakiendelea kumtukuza Mungu ukumbini

 hapo






Hii ni sehemu ya Umati uliohudhuria tukio hilo

Kutoka kulia ni Kijana anaitwa Josiah ambaye ni pekee


 asiye


 kuwa ndugu wa damu katika kundi hilo,Huyu Mkaka


 anaimba sauti ya nne ipasavyo.

Live Recording Ikiendelea

Hapa The Voice wakiimba pamoja na mmoja wa wapiga-


solo gitaa mahiri nchini Bro Sam Yonanyuma mwenye 


 Gitaa

Kiongozi wa kundi la The VOICE Bro Obedi, akimtambulisha mama yao Mzazi(The First Lady of The Voice), kwa umati uliokuwepo ukumbini hapo

ERICK BRIGHTON AAMUA KUOA: 
VIKAO VYAANZA

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI