KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Thursday, August 9, 2012

JE WAMTAMBUA NEYMA MUZYA MGAWE


YESU MTENDA MIUJIZA ANAZIDI KUTENDA MIUJIZA KILA ITWAPO LEO;;
BAADA YA KUPONA KATIKA AJALI YA PIKIPIKI NEYMA MGAWE MUNGU AMEWEZA KUMPA HUDUMA NA MAONO YA UIMBAJI NA SASA ANA NYIMBO AMEIMBA ILI KUKUONYESHA MUNGU ANAWEZA.
Huyu ndiye Neyma Mgawe akifurahia wema wa Mungu
Neyma Mgawe ndani vya viwanja Mlimani City.
Ndugu zangu naomba mnipokee katika huduma yangu hii ya uimbaji
KWA MAELEZO YAKE NEYMA MGAWE ANASEMA;;
Alianza kuimba akiwa bado mdogo na baada ya kusafiri kwenda kutembea Arusha kwa kaka yake Mungu alimpa kibali cha kuingia studio na kuimba nyimbo mbili ya kwanza ni Tenda muujiza na nyingine ni Mungu wa upendo.Anapendelea sana kuimba nyimbo za taratibu hasa za kuabudu,anapenda sana uimbaji wake ni Ephaim Sekeleti toka nchi Zambia.Neno ambalo alilopenda kuwaasa vijana wenzake anasema tumtafute Mungu maadam anapatikana pia tuache dhambi,anachukizwa sana na mavazi mabaya ambayo yanavaliwa na wadada wenzake.Wito wake kwa walio na vipaji basi wajaribu  kumwimbia yeye hata kama wanapita katika mapito magumu.Kuhusu albam yake anasema muda si mrefu na inawezekana kabla ya mwisho wa mwaka itakuwa tayari.Mwisho anasema anawatakia kila la kheri wadau wote wa  pamojakwaumoja2012.blogspot.com
Anatoka Mlandizi katika huduma ya KLPT Kisima cha Uzima


Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA

DARASA HURU LA UFAHAMU.

  NINI HUTOKEA KWA MKE KUFIWA NA MUME AU MUME KUFIWA NA MKE AU WAPENZI MMOJA KUFA!!

  Jambo la kwanza linalohuzunisha zaidi ambalo lina kiwango cha asilimia 100 ni mtu kufiwa na mke au mume. Rekodi zinaonesha kuwa, watu wanaofiwa na wapenzi wao huwa na huzuni kubwa kiasi cha kutishia maisha yao.

Msongo wa mawazo, mauzauza ni mambo ambayo yanatajwa kusababisha vifo vya ghafla na vya muda mfupi kwa watu waliofiwa na waume/wake zao, huku sababu ya vifo hivyo ikibaki kuwa ni msongo wa mawazo (stress).

Licha ya ukweli kwamba kufiwa mume/mke ni jambo zito lakini, huzuni inapokuwa ya kudumu kiasi cha kutishia maisha ya mtu, suala la uzembe wa kufikiri huchukua nafasi. Hivyo, ili mtu aweze kuepukana na matatizo yanayotokana na kufiwa ni lazima afuate muongozo ufuatao ambao utamsaidia kuipunguza au kuiondoa huzuni hiyo ambayo ni mbaya kuliko nyingine zote duniani. Kwanza, ni kukubaliana na ukweli kwamba mwenza amefariki na hatarudi, kulia na kuhuzunika hakusaidii. Pili ni kuziondoa taratibu kumbukumbu zote zinazokuja na kutawala mawazo kuhusu mkeo/mumeo aliyekufa. Usiyazamishe mawazo kwenye tukio hilo, ukiona kuwaza kunajitokeza ni bora kupuuza mawazo hayo kwa kutoyapa nafasi ya kukutawala. Usipende kukaa peke yako kwa muda mrefu. Usiangalie picha na kutembelea kaburi la marehemu mara kwa mara bila kuwa na sababu za msingi. Usivute taswira ya maisha mliyokuwa mkiishi zamani. Kaa karibu na watu uwapendao, tembelea sehemu zenye kuvutia. Epuka kuzungumzia mambo ya marehemu wako. Badili mazingira ya chumba mlichokuwa mkilala, kuwa bize na majukumu yako na andaa mipango ya kumtafuta mwenza mpya,
Yote kwa yote mpe Mungu nafasi zaidi ili kuyaepuka madhara yasije kukupata katika kuamua na kuchagua akufaae katika maisha yako

Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI