KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Friday, August 3, 2012

KATIKA MAISHA YA BINADAMU YAKO NA PANDE MBILI TOFAUTI AMBAZO NI KUPANDA NA KUSHUKA NDIYO MAANA KUNA USEMI USEMAO HUJAFA HUJAUMBIKA.JIFUNZE KUPITIA SEHEMU HII.
WAHENGA walisema hujafa hujaumbika na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Emmanuel Mwakisunga Jumamosi Juni13, 2004 alipopata pigo ambalo lilibadili kabisa mtazamo na mwelekeo wa maisha yake. Ajali mbaya ya gari ilisababisha apate jeraha kubwa shingoni, utumbo ukatoka nje, mguu wa kulia na mkono wa kulia vikavunjka mara tatu. Akiwa bado kijana mdogo mwenye miaka 22 tu, ndoto zake nyingi  zimeyeyuka kama barafu ndani ya moto mkali.

Hakutarajia hayo lakini hali ndivyo ilivyo, hivi sasa amepata ulemavu wa maisha.
 “Kwanza mimi kupona ni Mungu pekee, kwa sababu katika ajali ile nilinusurika mimi peke yangu wengine wote walikufa. Ilikuwa ni ajali mbaya sana, ambayo imenifanya niwe hivi unavyoniona.”  “Nimezaliwa Mbeya mwaka 1988, wazazi wangu wote ni wenyeji wa huko, tulizaliwa watoto tisa mimi nikiwa wa tano. Baba yangu ni mtumishi wa Mungu na mama yangu anafanya kazi za ndani kwa mtu,” anadokeza kidogo kuhusu familia yao.
Emmanuel alikomea darasa la sita baada ya kukosa karo ya shule alipata kazi ya utingo katika magari yatokayo Dodoma kwenda Morogoro. “Mwaka 2002 nilianza kazi hiyo ya utingo. Nashukuru kwamba ilikuwa ikinipatia senti mbili tatu ambazo zilinisaidia kula na kuvaa kwa sababu wazazi wangu hawakuwa wakijiweza kifedha,” anasema Emmanuel. Maisha yake yalibadilika akiwa na umri wa miaka 16 tu.

Siku hiyo basi lilikuwa limejaa pomoni na yeye akiwa utingo alikuwa amesimama mlangoni akihudumia abiria. “Tulijaza abiria siku hiyo hata nafasi haikutosha, mimi nilikuwa nimesimama mlangoni kama kawaida ya utingo. Tulikuwa tunatokea Dodoma tukielekea Morogoro majira ya saa kumi jioni. Gari letu lilikuwa linafukuzana na Fuso ambalo lilikuwa linataka kutupita.
Kusema kweli hakukuwa na sababu ya dereva wetu kukimbizana na Fuso lile, basi tu ilikuwa ni ujana na ujinga,” anasema Emmanuel na kuongeza:  “Gari letu likiwa katika mwendo mkali kupita kiasi ghafla mbele yetu tukaona lori aina ya Scania kubwa la mizigo likiwa linaelekea pia Morogoro, kwa kuwa gari letu lilikuwa katika mwendo mkali, lilishindwa kufunga breki, kwa hiyo likaingia nyuma ya scania hilo.
Wakati tukio hilo linatokea mimi nilikuwa nashuhudia kila kitu, nikataka kurudi nyuma ili niepuke kuumia kwa kuwa nilikuwa mbele, lakini ilikuwa ni vigumu kwa sababu gari lilikuwa limeshona.” Alisikia mlio mkubwa na sauti za vioo vikivunjika kisha likabinuka na kusererekea upande wa kushoto. Kutokana na kasi ile, alitupwa nje na bati moja lililotoka katika basi lao lilimwingia tumboni. “Nikarushwa nje hadi chini kwenye lami, bati likang’oka katika gari letu, likaniingia tumboni na kuzama kabisa nikawa najaribu kuling’oa lakini ikawa ni ngumu.
 Mpaka sasa sielewi lilitokaje, nikajikuta pembeni na nikawa nashuhudia utumbo wangu ukiwa nje.” “Mpaka nafikishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro  nilikuwa najitambua, nikawapa madaktari namba za simu za baba. Sikuwa nasikia maumivu, nilipofika mlangoni mwa hospitali tu, fahamu zikanipotea. Kwa mbali nikamsikia muuguzi akisema muwekeeni damu haraka.” Fahamu zilimrudia baada ya siku moja, wazazi wake walifika na kumkuta akiwa hoi, walimhamisha na kumpeleka Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
 “Tulipofika Dodoma madaktari wa pale walisema nimecheleweshwa sana, hivyo mkono na mguu vimeshaharibika na endapo wataviacha hivyo, basi uwezekano wa sumu kusambaa hadi kwenye moyo ni mkubwa na ungesababisha kifo changu. Baba na mama wakaulizwa kama wamekubali nikatwe mkono na mguu,
 Hawakuwa na la zaidi isipokuwa kukubali ili angalau wanione nikiwa hai.” Pamoja na wazazi wake kukubali, lakini bosi wake, mmiliki wa gari lililopata ajali, anayemtaja kwa jina la Mzee Kindole, hakutaka kusikia Emmanuel anakatwa mguu wala mkono, aliwaomba madaktari wajaribu njia nyingine za matibabu ili kijana huyo apone akiahidi kutoa gharama zote kwa kazi hiyo lakini haikuwezekana.

“Siku ambayo sitaisahau ni tarehe 20 mwezi wa sita, 2004, nilishtuka alfajiri nikawa nataka kwenda haja ndogo, nikajaribu kushusha mguu chini ili nitembee ukawa haushuki. Nikataka kushika mguu huo kwa mkono nao ukawa haufanyi kazi. “Baba yangu alikuwa pembeni yangu akaniambia: 'Usijali haya ndiyo maisha ambayo Mungu amependa uishi cha muhimu ni kuwa bado ungali hai.'
 
 Akaendelea kuniambia 'mwanangu Emma umekatwa mguu na mkono wa kulia.' Nililia sana sikuamini, nikatamani kufa lakini baba yangu alinitia moyo kwa kiasi kikubwa namshukuru sana.” Alikaa hospitali kwa miezi minne na alipopata nafuu aliruhusiwa, lakini kulingana na hali ya maisha ya familia yake, ilimbidi apigane na maisha, atafute mkate wake wa kila siku.
 Akaingia mtaani na kuanza kupiga debe kwenye daladala na ndipo alipwe ujira. Alikuwa akipata Sh200 au 100 kwa kila gari. “Wakati mwingine naomba barabarani lakini napenda zaidi kupiga debe kwa sababu kabla sijapata kilema nilikuwa nafanya kazi kwenye magari halafu sipendi sana kuomba watu fedha,” anasema. Emmanuel ni tofauti na walemavu wengi, anatamani afanye biashara kwa sababu hapendezewi na hali ya kuombaomba na kupiga debe. Kinachokwamisha yote hayo ni mtaji kwani pamoja na kubaki na mguu na mkono mmoja anasema anaweza kuuza nguo za kike na za watoto. Anapatikana kwa namba.


Mpaka hapa ninamatumaini kwamaba utakuwa umejifunza kitu toka kwa Emmanuel
Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA


SOLOMONO MKUBWA KUANZISHA KITUO CHA WATOTO YATIMA



TAMASHA KUBWA KUFANYIKA NDANI YA CCC
.Asante Asante Concert  na 
SOLOMON MKUBWA ni tamasha la kurudisha fadhila kwa watanzania wote kwa kujenga kituo kikubwa cha kulelea watoto yatima  tamasha hilo itakua kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa kituo hicho maeneo ya 
BUNJU "A"  DAR ES SALAAM
TAMSHA HILI ITAKUA NI  JUMAPILI YA TAREHE  19/08/2012
NDANI YA UKUMBI WA CITY CHRISTIAN CENTRE;C.C.C /UPANGA DAR ES SALAAM
MUDAA: KUANZIA SAA  8 MCHANA NA KUENDELEA
Kiingilio ni 10.000 V.I.P
                  5000 Viti maalum
                  3000 watoto
waimbaji wote watakao shiriki ni kama vile: CHRISTINA SHUSHO
  UPENDO NKONE
  BONIE MWAITEGE
 UPENDO KILAHIRO
 JENIPHER MGENDI
 TARAJA NTAMBOBA
 NA WENGINE WENGI WAIMBAJI WOTE WATA SHAMBULIA JUKWAA LIVE
NUNUA TIKETI YAKO NA FAMILIA MAPEMA ILI KUEPUKA KUKAA FOLENI KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU NO.
0713981393
0762804600
AMA  NENDA CALVARY TABERNACLE CHUCH KINONDONI KARIBU NA MAHAKAMANI ,CCC UPANGA, WAPO RADIO ,PRAISE POWER RADIO, NA CLOUDS FM
TAMASHA  HILI LIMEDHAMINIWA NA
AG/PRESS,WAPO RADIO ,CLOUDS FM&TV,CITY CHRISTIAN CENTRE /UPANGA  NA  PAMOJA KWA UMOJA.
Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA

NYUMBA YA MPENDWA INAPANGISHWA.

NYUMBA NYUMBA!!!  INAPANGISHWA KWA BEI NAFUU SANA NYUMBA YENYE HADHI(KIWANGO)KUBWA MAENEO YA SINZA KWA REMMY.0715408566

Hapa ni ndani koridoni

Hapa ni koridoni kwa mbele ukiwa stin' room

Hapa ni jikoni na majiko ya gesi kama yanavyoonekana katika picha.

Hapa stin'room na hii ndiyo roof ya Gpsum.mable.
Hiki ni chumba cha nje ambacho waweza kifanya ofisi au mambo ya salon kwa ajili ya familia,ambacho kiko kama kighorofa fulani.

Hii ni sura ya mbele ya nyumba yenye eneo kubwa kwaajili ya packing ya magari matatu

Hii ni sura ya ubavu wa kulia mwa nyumba ambako unaona kuna heater ya kuchemshia maji yakuoga ama kufutia ambazo ziko kila chumba pamoja na AC.

Hii ni sura ya mbele karibu na gate kama picha inavyoonyesha

Hili ni eneo la nyuma ya nyumba kama panavyoonekana

Huu ni ubavu wa nyumba upande wa kushoto kama panavyoonekana.

 Huu ni mwonekano wa nyumba kwa sura ya nje kama picha 
Nyumba hii inakodishwa  na mpendwa mwenzako ambaye alimwombaMungu ampe nyumba ya biashara ya kupangisha,Na Mungu akampa.Nafasi iko wazi kwa wewe unayehitaji kujitangaza kupitia blog hii ya kikristo Tanzania,Nafurahi sana napokuona wewe ukiifanya blog hii kuwa ni madhabahu ya Mungu baba.Katika maombi tumekuwa tukimwomba Mungu na yeye amekuwa akitupa,mwenzetu huyu Mungu amemjibu pia endelea kuwaombea wote walio fanikiwa kupitia Maombi ya kila siku bado hata wewe inawezekana ukimtumaini Mungu baba.Kwa maelezo zaidi kuhusu nyumba hii piga simu no 0715 408566

Rafiki bado ninakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA.

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI