KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Thursday, August 16, 2012

DARASA HURU LA UFAHAMU


                  KANUNI ZA KUIFIKIA FURAHA YA KWELI
Wakati wa kutafuta furaha ya kweli lazima kujiuliza baadhi ya kanuni za kimaisha kama unazifuata kwa ufasaha, vinginevyo unaweza kuwa mtafuta furaha lakini usiwe miongoni mwa wanaoipata. Kama nilivyosema awali kuwa, kuna watu hutafuta furaha kupitia kwa wake/waume zao, rafiki, wapenzi na hata kwenye mali, lakini mwisho wa siku wanapokuja kutafakari zaidi hujikuta hawana furaha waliyoitaraji wakati wakihangaikia njia za kuipata.
Kuna watu ambao mawazo yao yanatamani sana kupata mtoto na wengine wameapa kabisa kwamba wakifanikiwa kushika ujauzito watakuwa na furaha, lakini bado kama hawatakuwa makini wao wenyewe watajikuta wanapata furaha ya muda na hatimaye kutoweka na kuanza kujutia harakati zao, huku wakianza safari mpya za kufuata furaha kupitia jambo jingine. Hebu tujiulize maswali haya.
A-Je tunapokuwa tunatafuta furaha tunatumia uwezo wetu wote au kwa kiwango kidogo? Kama tunatumia kiwango kidogo basi tujue kuwa hata kama tutapata kitu tunachodhani kitatufurahisha utajikuta hatufurahi, kwa sababu hatutafanikiwa au tutakuwa na furaha ya muda tu kwa vile nia yetu hatukuijaza kikamilifu ili tuweze kupata furaha timilifu
B- Je tunafanya sawa katika maamuzi au tunabahatisha tu? Endapo tutakuwa tunafanya mambo ya kubahatisha ambayo hatujayahakiki, huzuni yetu itakuwa kwenye makosa na kamwe hatuwezi kufanikiwa kupata yale tunayotaraji yatufurahishe. Kuna watu wanatafuta watoto lakini hawazingatii kalenda za mimba na wengine wanatafuta mali, elimu kubwa, mke mwema, lakini hawako makini katika kufanya maamuzi kwa usahihi. Ni vema tukathibitisha uchaguzi wa mambo ili tufanikiwe kupata yatakayotufurahisha.
C- Je tunatimiza wajibu wetu au tunadanganya? Wapo watu ambao walitamani kuoa ili wapate furaha, lakini walipofanikiwa katika hilo hawakutimiza majukumu yao wakajikuta wanageukwa na wake/waume zao na kujutia uamuzi wao. Msomaji wangu, unapokuwa katika safari ya kutafuta furaha kupitia utajiri, elimu, uongozi ni vema ukatimiza wajibu wako, ili upate matokeo mazuri. Maana kama utakuwa unatamani kufaulu mtihani wako halafu husomi kwa bidii, sina shaka majibu utakayopata yatakuhuzunisha kwa sababu lazima ufeli na furaha uliyotaka haitapatikana.
 D- Je tunafuata muongozo, au tunakiuka? Kila jambo tunalotaka kulifanya lina kanuni zake, ukitaka kupika ugali upo muongozo ambao unakutaka uwe na vifaa, uache maji yachemke na hata kutoharakisha upishi wenyewe, lengo ni kupata matoke mazuri. Sasa kama tutakuwa kupata furaha ya kudumu kupitia mambo fulani ni lazima tuyafanye kwa kufuata muongozi na si kwa kukurupuka. Biashara, elimu, kazi, zote hizi zinamiongozo ambayo lazima kuifuata kwa matokeo mazuri.
 E- Tunatumia tulivyopata au tunavitelekeza? Wapo watu ambao hutamani kupata kazi, lakini wanapopata hawazitumii, kazi hizo kwa ukamilifu, badala yake wanakuwa watu wa kufanya ujanja ujanja ujanja kwa kutoroka na wakati mwingine kutojihusisha na shughuli nyingine kwa lengo lile lile la kutafuta furaha. Kusema kweli mtu wa namna hii hawezi kuwa na furaha kwa sababu anayolenga yamfurahishe hayatumii kufurahika na badala yake anatafuta jambo jingine. Fikiria kuhusu mume, anaoa lakini anaacha kumtumie mke wake wake anakwenda kwa hawara! Hili si jambo jema na kamwe haliwezi kuleta furaha kupitia mambo tunayoyatafua. Soma vifungu hivi ndani ya kitabu cha Biblia: “Vitu vyote ni halila, bali si vitu vyote ifaavyo.
 (1 Wakorintho 10:23).” “ Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi (Yakobo 4:17)
   
Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI