KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Wednesday, September 12, 2012

DARASA HURU LA UFAHAMU

KUJERUHIWA  AMA  KUUGULIWA.


Watu wengi wanapojeruhiwa hasa vibaya au kupatwa na magonjwa sugu yanayotajwa kuwa hayana tiba hufadhaika sana. Mgonjwa kama kansa, kisukari, ukimwi, BP yamewahuzunisha wengi, hii inatokana na hofu ya kufa, ingawa ukweli unabaki kuwa kifo hakina ushirika na magonjwa hayo tu kwani kuna wanaokufa bila kuugua magonjwa hayo.
Jambo kubwa la kufanya ni kuondoa hofu kwa kuchukua mifano ya watu ambao wameishi/wanaishi kwa muda mrefu wakiwa na magonjwa hayo, lakini hawajafa. Usijifananishe na waliokufa mapema kwani inawezekana walikuwa na hofu ndiyo maana wakafa. Hofu ndiyo inayotajwa kuua watu wengi kuliko hata magonjwa yenyewe.  Acha kufikiria mawazo ya kufa, usikate tamaa, endelea kufanya mambo yako kama kawaida na uwe karibu na watu wa kukufariji si wa kukuvunja moyo.
Usijihukumu kuwa ni mkosa mbele ya jamii na usione kama umeonewa na Mungu. Tembelea wagonjwa wengine hospitali, huko utaona wenye shida zaidi yako, hiyo itakupa unafuu wa kubeba udhaifu wako. Kwa wale waliopata ajali ni vema wakakubaliana na matokeo, wakatulia na kuwatembelea watu wenye ulemavu ili kupata msaada wa kimawazo na wakati mwingine kufanya ibada ya kuomba wapewe uvumilivu.
 Ifahamike kuwa, ulimwenguni kuna walemavu wengi ambao wana maisha mazuri kuliko hata wazima, hivyo basi kuwa kilema haimaanishi kuwa umefikia mwisho wa maisha.
NDUGU YANGU USILIE WALA KUKATA TAMAA MUNGU BADO ANAWEZA KUBADILISHA HISTORIA YAKO AMINI KUANZIA SASA KUWA INAWEZEKANA
Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA


ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI