KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Sunday, August 12, 2012

DARASA HURU


 JE!!! NINI KIFANYIKE FURAHA YA KWELI UIPATE??
Watu wengi wanapopata matatizo huwa hawakubali kuyapokea. Kuna mfano wa mtu mmoja ambaye alikuwa bosi katika kampuni, siku moja uongozi wa juu uliamua kumshusha cheo kutoka ukurugenzi hadi mpokea wageni. Bosi huyo alipotelemshwa cheo kwa kiwango hicho hakujiona duni kwa wafanyakazi wenzake, badala yake alichofikiri yeye ni kwamba watu wote wanamuunga mkono na kumsikitikia kwa unyama huo wa kushushwa cheo kupitiliza.
Zile fikra za kuhurumiwa na watu zilimfanya awe na furaha na akawa mtu wa kuwahi kazini kila siku ili watu wakamuone na kumsikitia, jambo ambalo aliamini kuwa uongozi uliomshusha cheo ndiyo unaopata aibu mbele ya jamii na wala sio yeye. Kitendo hicho cha kuwahi kazini na kuonekasna ni mtu mwenye furaha kilimfanya awe mtu wa pekee kwenye jamii, aliweza kutengeneza maswali mengi kwa watu na hatimaye minong’ono ya kuonewa ilianza kusikika.
Kilichotokea hatimaye, kampuni moja kubwa ilipata habari ya kuwepo kwa mtu wa aina hiyo, ikafanya mawasiliano naye na kumwajiri, bila kujali kashfa zilizokuwa zimemwengua katika wadhifa wake wa kwanza. Jamaa huyo alipopata ajira mpya alijirekebisha makosa yake ya kugushi na wizi kwa vile alikuwa amejifunza kilichokuwa kimempata. Bosi huyo aliweza kuendesha kampuni hiyo kwa mafanikio makubwa, jambo lililowafanya wakuu wake wa zamani wajute kumuondolea wadhifa.
Hapa tunajifunza kuwa tunapopata matatizo kinachotufanya tupoteze furaha ni fikra zetu, lakini tukijua kucheza nazo na kuzielekeza katika mlango wa pili, tunaweza kuyatumia matatizo yetu kupata furaha pia. Lazima kila mmoja wetu atambue kuwa matatizo ni shule, tunapoyapata tunajifunza. Lakini hatuwezi kujifunza tukiwa na msongo wa mawazo, lazima tufanye unafiki fulani wa kimawazo kama alioufanya bosi aliyeshushwa cheo, yeye hakuangalia wadhifa wake wa zamani, wala namna gani watu wanamtazama katika kazi yake mpya. Mawazo yanawezaje kutuletea furaha?
Katika hali ya kawaida hakuna mtu hata mmoja anayeweza kumwambia mwenzake lia naye akafanya hivyo. Kila siku tunaona na kusikia mengi kutoka  kwa ndugu, rafiki, waalimu wahubiri, wachungaji mapadri wetu na hata kwenye vyombo ya habari, lakini kusikia huko hakuna maana kuwa ni lazima kutuondolee furaha, kwani ndani ya akili zetu kuna kitu muhimu ambacho ni maamuzi yetu.
Utawala wa mawazo yetu ni kazi ya kila siku na uamauzi wa nini ha kufikiri ni suala ambalo lipo kwenye uwezo wa mwanadamu mwenyewe. Ingekuwa ni lazima kila wazo baya tunaloliona na kulisikia lazima lituhuzunishe basi tusingekuwa na furaha hata kidogo katika maisha yetu, kwani hakuna siku ambayo itapita bila kuona, kusikia au kutendewa jambo baya na mtu mwengine.
Ajali zinatokea kila siku, watu wanakufa, wanaugua, wanateseka, wanalia, wanaomboleza na kufanyiana hila, lakini kwa nini hatuyachukulii matukio yote kwa uzito sawa kiasi ha kulia? Ni kwa sababu tuna uhuru wa kuchagua tulie kwa sababu ya nani na kwa nina? Na hii ndiyo silaha pekee ya kuyatumia mawazo kutuletea furaha. Yaani kuchagua lipi la kutuliza na lipi la kutufurahisha na mwisho wa yote tuna uwezo wa kuyatumia mawazo yetu kuchagua mambo ya kufurahisha na kuyapa kipaumbele, bila kujali ni mema au mabaya. (Kumbuka mfano wa bosi aliyeshushwa cheo).
Hivyo ni vema wakati tunapokuwa na mawazo ndani yetu tukazingatia misingi ifuatayo ambayo inaweza kutusaidia kufikia uamuzi sahihi juu ya kila tunaloona na kulisikia, ili mawazo yasitufanye tuhuzunike na badala yake tufurahi. Kwanza ni kujipenda wenyewe. Tukijipenda hatutajihukumu na kujiona duni mbele ya wenzetu na hivyo kutopoteza furaha. Pili ni kujiamini, kuamini huku kutatuwezesha kuwa na msimamo juu ya maamuzi ya kila tunachoshibishwa ndani ya mawazo yetu kupitia mawasilia ya sauti na yasiyo na sauti.Tatu, kumiliki mawazo yetu yasichukuliwe na ukubwa au udogo wa tatizo. Udhibiti huu lazima uyaone mambo yote yanayoingia kichwani kuwa ni ya kawaida kwa vile yapo duniani na yanawakuta watu kama sehemu ya changamoto za kimaisha. Katika hali ya kawaida ukubwa au udogo wa tatizo unatokana na mawazo ya mtu husika. Nne, kuwa na uvumilivu juu ya kila jambo kwa imani kuwa hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Tano na mwisho ni kuhakiki maamuzi yako kama yako sahihi kabla na baada ya.
Rafiki bado nakuombea Mungu akubariki
PAMOJA kwa UMOJA

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI