KARIBU

KARIBU UPATE HABARI MBALIMBALI KUPITIA BLOG HII;;pamojakwaumoja2012.blogspot.com.
AU PIGA simu 0715408566 kwa Ushauri na maoni

KAULI MBIU/SLGN


HOPES

Tuesday, July 24, 2012

RAIS GHANA AFARIKAI DUNIA GAFLA


             Rais wa Ghana John Attah Mills afariki
Imebadilishwa:                         25 Julai, 2012 - Saa 17:51

Taarifa kutoka afisi ya rais zinasema kuwa alifariki

 ghafla baada ya kupelekwa hospitali siku ya

 jumatatu. 
Taarifa zinazohusiana
  •  
Msaidizi wake pia amethibitisha kufariki kwa

 kiongozi huyo.
Kifo cha rais wa taifa la pili duniani kwa ukuzaji wa

 cocoa kimekuja wakati alikuwa anajiandaa

 kupogania tena urais.
Rais Attah Mills ambaye husafiri mara kwa mara

 kwenda ng'ambo kwa matibabu alifariki muda mfupi

 baada y kupelekwa katika hospitali moja mjini

 Accra , Ghana.
Ni hivi majuzi tu rais huyo alisafiri hadi Marekani

 kwa kile kilichosemekana kwa ni uchunguzi wa

 kawaida wa afya yake.
Kwa muujibu wa katiba ya Ghana, Makamu wa Rais

 John Dramani Mahama anatarajiwa kushikilia

 hatamu za uongozi hadi uchaguzi wa urais

 utakapofanywa.
Ghana ilikuwa inatarajiwa kwenda katika uchaguzi

 mkuu mwezi Disemba mwaka huu ambapo John

 Attah Mills alikuwa ametangaza nia yake ya kutete

a uadhifa wake.
Wakati wa uongozi wake, uchumi wa Ghana

uliimarika na demokrasia kupanuka zaidi.
" Ni kwa masikitiko makuu na kwa moyo mzito...

 Tunatangaza kifo cha ghafla cha rais wa jamhuri ya


 Ghana " taarifa iliyotumiwa shirika la Reuters

 kutoka ofisi ya rais ilisema.
Tarifa hiyo ilisema kuwa Rais Mills mwenye umri wa

 miaka 68 alifariki saa chache tu baada ya kupelekwa

 hospitali.
Hata hivyo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Lakini msaidizi wake mmoja ambaye hakutaka

kutajwa, alisema kuwa Rais John Attah Millis

alisikika siku ya Jumatatu akilalamika kwa

 anaumwa.
Hali yake ilizorota na hatimae kufariki mapema siku

 ya Jumanne.

Bwana alitoa,bwana  ametwaa.

No comments:

Post a Comment

ABEDDY NGOSSO/SARA K

FANUEL SEDEKIA NA UPENDO WA YESU-MUNGU AKUBARIKI